Sunday 20 November 2016

TANZANIA YAZINDUA MAGEUZI YA LESENI ZA BIASHARA




NA SOPHIA KESSY

Serikali ya Tanzania imezindua mpango wa mageuzi ya leseni za biashara ili kuwarahisishia wawekezaji kupata huduma zenye ufanisi kwa haraka zaidi nchini humo. 

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji  Charles Mwijage amesema kuwa lengo ni kuvutia wawekezaji na kuongeza ufanisi na kuboresha utaratibu wa sasa wa leseni za biashara na kutoa vibali hapa nchini wakati serikali ya Tanzania ikiwa katika mchakato wa kukuza sekta ya viwanda. 

Mwijage amebainisha kuwa, mpango huo utakutanisha bodi ya wataalamu kutoka kwa wananchi pamoja na sekta binafsi ili kuandaa mpango kazi ambao utasaidia mazingira bora ya uwekezaji.

No comments:

Post a Comment