Sunday 13 November 2016

WAKULIMA WA BAMIA MKOANI TANGA WAOMBA KUWEZESHWA



NA SOPHIA KESSY..


Shamba hili la  kilimo cha bamia liko pembezoni mwa barabara ya Tanga horohoro  eneo la Kisosora kata ya nguvumali jijini Tanga likiwa na ukubwa wa hekari tano, hapa ndipo wakulima hawa wadogo wanapoendesha kilimo kwa kukodi ardhi kwa msimu.

Licha ya juhudi kubwa za wakulima hawa, changamoto yao kubwa ni ukosefu wa mbegu bora, upatikanaji wa wataalamu na soko la uhakika litakalowaondoa katika hali ya utegemezi.

Ili kupaza sauti zao IBER inafika katika eneo hilo na kuzungumza na Bibi AZINATI HIYOBU  , AMINA BAKARI na FADHILUNA YAHAYA ambao licha ya umri wao mkubwa ndoto zao ni kuondokana na jembe la mkono.

Akijibu hoja hiyo Afisa Kilimo Kata ya Mafisa Mkoani humo amesema  amewataka wakulima kubadilika na kuachana na kilimo cha mazoea  na badala yake watumie elimu kutoka kwa wataalam kujiendeleza.

Ili wakulima hawa kuweza kutimiza ndoto zao ni vema taasisi za kifedha kupunguza masharti ya mikopo ili wajasiriamali hawa waweze kukopesheka na kujinunulia pembejeo zao wenyewe.

No comments:

Post a Comment